Social Icons

ad3

ad3

ad2

ad2

ad1

ad1

Saturday, February 24, 2018

MAKUFULI KUFUNGWA KESHO MBEYA



  Mashabiki mbalimbal;i wakiwa wamefurika kwenye uwanja wa Tandale mjini Tukuyu.(Picha kwa hisani ya dinaismail.blogspot.com)
*Tukuyu wangoja majaliwa kupanda daraja

* Ifisi yasubiri suluhu


NA GORDON KALULUNGA, RUNGWE


LIGI daraja la Tatu ngazi ya Mkoa wa Mbeya hatua ya timu sita bora, inatarajiwa kutia nanga kesho katika viwanja mbalimbali huku ubingwa ukinukia kwa timu mbili ambazo ni Tukuyu Star (Banyambala) na Ifisi Hospital FC (Wadunga Sindano).



Mechi hiyo ambayo inatarajiwa kupigwa kesho katika uwanja wa Tandale uliopo mjini Tukuyu wilayani hapa, imekuwa gumzo katika mitaa mbalimbali ya wilayani Rungwe vikiwemo vijiwe kadhaa katikati ya mji huu wa Tukuyu.



Timu ya Tukuyu Star ili kupata ubingwa huo wa Mkoa wa Mbeya, inahitaji kuifunga timu ya Ifisi ambayo ina pointi 10 dhidi ya pointi 9 za wenyeji Tukuyu Star.



Wakati wenyeji Tukuyu wakiwa wanafanya kila aina ya ufundi wa kuweza kushinda mechi hiyo ya kesho, timu ya Ifisi FC wao wanahitaji kupata suluhu ya aina yeyote kisha kubeba ubingwa huo na kupanda daraja kuelekea daraja la pili.



Wachezaji wa timu ya Ifisi ambao tayari wametinga mjini Tukuyu jana, leo asubuhi wameonekana katika uwanja wa Katumba Two ambako taarifa zisizorasmi zinasema kuwa mtanange wa timu hizo unaweza kuhamishiwa katika uwanja huo kutoka Tandale.



Mpaka sasa msimamo wa ligi hiyo inajiweka wazi kuwa Ifisi Hospital FC ina pointi 7, Tukuyu Star pointi 9, Iduda FC pointi 7, Yosso FC pointi 3, Syukula FC pointi 3 na Ilomba FC pointi 0.

No comments: