Social Icons

ad3

ad3

ad2

ad2

ad1

ad1

Sunday, June 10, 2018

LESENI ZA UCHIMBAJI ZILIZODUMAA BILA KUFANYIA KAZI CHUNYA KUNYANG'ANYWA




 
Na Mary  Mwaisenye, Chunya.

Baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Chunya mkoani Mbeya limekubaliana kupitia kuhakikisha wanayanyang'anya makampuni yote yaliyo shikilia leseni za tafiti kwa muda mrefu ili wachimbaji wadogo waweze kuyatumia maeneo hayo.

Makubaliano hayo yalifikiwa katika kikao cha robo ya Tatu kilichofanyika jana ambapo walisema wachimbaji wadogo wadogo wa madini ya dhahabu wamekuwa wakinyanyaswa na wachimbaji ambao wamekuwa wakishika leseni bila kuyatumia maeneo waliyopewa.

Akizungumza katika kikao hicho mbunge wa jimbo la Lupa Victor Mwambalaswa, alisema hawezi kuona wachimbaji wadogo wadogo wilayani kwake wakiwa wananyanyaswa na wachimbaji wakubwa ambao wamekuwa wakishikiria leseni kwa muda mrefu bila kuzitumia na kusubiri mchimbaji mdogo avumbue maeneo yenye dhahabu ndipo wanajitokeza na kusema ni maeneo yao.

Alisema yeye  kama kiongozi atahakikisha anamshauri waziri mwenye dhamana kuhakikisha wale walioshikiria maeneo hayo kuazia mwaka 2005 hadi sasa wanawaachia wachimbaji wadogo ili waweze kuyatumia ili kuepusha migogoro kati ya wachimbaji wadogo kwa wakubwa.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Chunya Noeli Chiwanga alisema kuna haja ya serikali kuu kuhakikisha wanawatazama wachimbaji wadogo kwa jicho la tatu kutokana na kwamba wao ndio walioko maeneo husika na ndio wavumbuzi wakubwa wa maeneo hayo yalio na leseni lakini wanapochimba wanaambiwa eneo hilo lina leseni na mwenye leseni yuko Dar es salaam na wachimbaji wadogo kufukuzwa.

Chiwanga alisema kama mwenyekiti wa chama hafurahishwi kabisa na wachimbaji wadogo kufukuzwa katika maeneo ambayo wamekuwa wakiyavumbua hivyo anakubaliana na maamuzi ya baraza hilo la Madiwani kuazimia leseni za muda mrefu kufutwa.

Awali akifungua kikao hicho Mwenyekiti wa Halmshauri Bosco Mwanginde alisema kama baraza lazima waungane kwa pamoja katika kusimamia sheria na mipango yote inayowekwa baraza lao ili kuhakikisha maendeleo ya halmshauri yanasonga mbele.

Mwanginde alisema  pamoja na kuiomba serikali kuu kuzifuta leseni za muda na kupewa  wachimbaji wadogo wadogo pia aliomba madiwani kuhakikisha wanawaelimisha wachimbaji wadogo wadogo kuhusiana na tozo zilizowekwa na Halmshauri ili waone kulipa tozo hizo ni uzalendo katika kujenga wilaya yao.

Mwanginde pia alisisitiza madiwani kusimamia watendaji wa kata na vijiji kusimamia mapato hasa katika kipindi hiki cha mavuno ili waweze kukamilisha vyema robo iliyobakia ambapo alisema kwa sasa wamefikia 73%.
 
Mkuu wa wilaya ya Chunya Rehema Madusa akiwasilisha salamu zake kwa madiwani aliwataka watendaji wa halmshauri kuwa wabunifu wa vyanzo vya mapato ili kuongeza mapato ya Halmshauri na kufikia malengo yaliyowekwa na Serikali kuu.

Madusa pia aliwataka Madiwani kuhamasisha wananchi katika suala la maendeleo hasa katika ujezi wa madarasa na vyumba maalum vya wasichana wanapokuwa katika hedhi ili wasiweze kupoteza vipindi darasani.

No comments: