
Kwa upande wa Tanzania, serikali inatarajia kutumia jukwaa hilo kuhimiza ufadhili na ushirikiano katika sekta ya nishati safi, hususan miradi ya gesi asilia, umeme wa jua na matumizi ya majiko banifu.
“Kupitia COP30, tunatarajia kuhamasisha uwekezaji katika nishati safi na kuhakikisha kaya nyingi nchini zinatumia nishati rafiki kwa mazingira.”
Tanzania pia itawasilisha taarifa yake kuhusu utekelezaji wa Nationally Determined Contributions (NDCs) – ikilenga kupunguza uzalishaji wa gesi chafu kwa zaidi ya asilimia 30 ifikapo mwaka 2030.
Aidha, nchi inatarajia kupata ufadhili wa kimataifa kusaidia miradi ya upandaji miti, uhifadhi wa misitu, na uboreshaji wa upatikanaji wa umeme wa jua vijijini.
Wakati dunia ikiendelea kutafuta suluhisho la mabadiliko ya tabianchi, Tanzania inaiona COP30 kama fursa ya kuchochea uchumi wa kijani na kukuza ajira kupitia sekta ya nishati safi.
Huo ulikuwa mwangwi wa Tanzania kuelekea mkutano wa COP30 unaotarajiwa kufanyika Brazil.



0 Comments