Dkt.Tulia ametembelea na kukagua maeneo yote katika kata za Ilemi na Isyesye ambayo athali kubwa imetokea na kuahidi kuwasilisha changamoto hizo kwa serikali ili wananchi hao waweze kupatiwa msaada wa haraka kabla ya athali hizo kuwa na matokeo makubwa.
Dkt. Tulia amewataka wananchi kutokujenga maeneo ambayo yanachangamoto ya kujaa kwa maji lakini pia kwa wale wanaotupa taka katika mifereji ya maji waweze kuacha tabia hiyo kwani inapelekea mifereji hiyo kuziba na kupelekea maji kuongezeka na kuleta maafa kwa baadhi ya wananchi.
Dkt. Tulia amehitimisha kwa kuwapa pole wananchi wote wa kata hizo hasa waliokumbwa changamoto hiyo kwa kipindi ambacho unatafutwa ufumbuzi wa kutatua changamoto hiyo.



0 Comments