MAHUNDI ATUA LUSAKA ZAMBIA APOKELEWA NA BALOZI MKINGULE

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya habari Mhandisi Maryprisca Mahundi (Kushoto) amewasili Lusaka nchini Zambia kushiriki Katika Mkutano wa The ( Digital Government Africa).

Mhandisi Mahundi amepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Zambia Ltn.Gen. Mathew Mkingule ambapo mkutano huo ni utafanyika kuanzia Oktoba 2 hadi 4 2024.

Katika safari hiyo Mhandisi Mahundi ameongozana na maafisa waandamizi watatu kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya habari.




Post a Comment

0 Comments