MHANDISI MAHUNDI AMEWAELEKEZA TTCL KUTANGAZA HUDUMA WAZITOAZO

 


NAIBU Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Maryprisca Mahundi amelielekeza shirika la mawasiliano  Tanzania  (TTCL) kuhakikisha linatangaza, na kutoa elimu Kwa  jamii  juu ya huduma zinazotolewa na Shirika hilo.



Ameyasema hayo leo12 Oktoba ,2024  alipo tembelea makao Makuu ya  Shirika hilo yaliyopo Mtaa wa Samora jijini Dar es salaam wakati wa ziara yake ya kutembelea shirika hilo lengo likiwa ni kujua jinsi linavyo fanya shughuli  zake.

" Nawaelekeza TTCL , Huduma kama simu za mezani , T-pesa ziendelee kuboreshwa, pamoja na maeneo yote  ya muhimu mtandao usisumbue mfano maeneo hayo ni pamoja na kwenye mifumo ya malipo ya Serikali, katika station zote za SGR na mengine."

Hata hivyo Mhandisi Mahundi  pia amelipongeza shirika la TTCL kwa huduma  nzuri ya fiber mlangoni. Na ameliomba Shirika hilo kuongeza ubunifu katika huduma hii,Ili waweze kwenda sambamba na Taasisi zingine zinazo toa huduma kama hii.

Post a Comment

0 Comments